Artwork

Inhalt bereitgestellt von UN Global Communications (Digital Solutions Unit) and United Nations. Alle Podcast-Inhalte, einschließlich Episoden, Grafiken und Podcast-Beschreibungen, werden direkt von UN Global Communications (Digital Solutions Unit) and United Nations oder seinem Podcast-Plattformpartner hochgeladen und bereitgestellt. Wenn Sie glauben, dass jemand Ihr urheberrechtlich geschütztes Werk ohne Ihre Erlaubnis nutzt, können Sie dem hier beschriebenen Verfahren folgen https://de.player.fm/legal.
Player FM - Podcast-App
Gehen Sie mit der App Player FM offline!

Wiki mbili za kusaka usalama DRC, mkimbizi asimulia madhila na atakacho.

2:23
 
Teilen
 

Manage episode 444122748 series 2027789
Inhalt bereitgestellt von UN Global Communications (Digital Solutions Unit) and United Nations. Alle Podcast-Inhalte, einschließlich Episoden, Grafiken und Podcast-Beschreibungen, werden direkt von UN Global Communications (Digital Solutions Unit) and United Nations oder seinem Podcast-Plattformpartner hochgeladen und bereitgestellt. Wenn Sie glauben, dass jemand Ihr urheberrechtlich geschütztes Werk ohne Ihre Erlaubnis nutzt, können Sie dem hier beschriebenen Verfahren folgen https://de.player.fm/legal.
Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC, imesalia katika mgogoro kwa miaka mingi, hali ambayo imewasababishia raia mateso ya hali ya juu zaidi yakiwemo mauaji, utekaji nyara, na kuteketezwa kwa nyumbaa zao. Mapigano hayo pia yamewafungisha viragozaidi ya watu milioni 6.4 nchini humo, na kulazimisha familia kutafuta usalama katika makazi ya muda yaliyojaa pomoni. Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi UNHCR limeonya kuwa mgogoro huu uliodumu kwa muda mrefu na ukiukwaji wa haki za binadamu ni mwiba kwa wakimbizi hawa wa ndani. Cicey Kariuki na taarifa zaidiRusayo ni eneo lililo na makazi ya muda ya wakimbizi mjini Goma katika Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Kongo. Miongoni mwa wakimibizi wa ndani wanaishi kwenye makazi haya ni Sebororo, mwanamke mwenye miaka 38 akitembea na watoto wake.Sebororo pamoja na wananawe watano wanaishi kwenye makazi ya pamoja na familia nyingine 90 huku wakisubiri kutengewa nyumba katika eneo hilo. Mama huyu anaeleza jinsi alivyojikuta katika makazi ya wakimbizi. Anasema,“tulianza kukimbia kuktoka kule tarehe tano mwezi wa kumi, awali walikuwa wanakuja lakini hawakuua watu, lakini leo hii wanaua watoto,wanaume na wanawake, sisi yalitushinda maanake wengine walikuwa pia wanatekweteza mimea.”Sebororo na watoto wake watano walitembea kwa wiki mbili kutafuta usalama, baada ya wapiganaji kuvamia kijiji chao cha Kiseguru katika Mkoa wa Kivu Kaskazini. Katika nusu ya kwanza ya mwaka wa 2024 pekee, zaidi ya watu 940,000 walilazimika kukimbia kutokana na ukatili, uliofanywa na makundi mengi yenye silaha yasiyo ya kiserikali huku familia nyingi zikifurushwa mara kadhaa. Kwa sasa anachokitamani zaidi Sebroro ni amani. “Haja yetu sisi ni watusaidie kwa kusimamisha vita ili turejee kwetu kwa sababu watu wanaisha.”Anasema.Kufurika kwa watu katika makazi haya ya muda kumezua wasiwasi mkubwa miongoni mwa wahudumu wa kibinadamu kufuatia hatari ya kuenea kwa magonjwa, ikiwa ni pamoja na virusi vya homa ya nyani au mpox.Ruven Menikdiwela, Kamishna Msaidizi wa Operesheni wa UNHCR ambaye alitembelea eneo hilo na kukutana na familia mbalimbali za wakimbizi na kusikiliza wasiwasi wao, anasema, “leo asubuhi, nilizungumza na mwanamke huyu ambaye ana watoto wadogo watano. Alitembea kwa wiki mbili kufika katika eneo hili, bado anasubiri huduma, bado anasubiri watoto wake watibiwe, na bado anasubiri chakula. Ninatambua kwamba hii ni hali ya kawaida kwa watu wote wanaoishi katika eneo hili. Kila mmoja ana majanga yake binafsi, kwa hivyo hizi siyo tu takwimu, bali kuna hadithi za kibinafsi nyuma ya kila moja ya hizi takwimu na majanga ya kibinafsi na majanga yanayoendelea pia, kwa sababu hatuoni suluhisho lolote kwenye mustakabali.”Katika ziara yake kwenye makazi haya, Ruven Menikdiwela, pia alifanya vikao na wadau kadhaa akiwemo Waziri mkuu, mamlaka za mkoa na mashirika ya umoja wa Mataifa. Ujumbe wake ulikuwa wazi kwamba amani ndiyo suluhisho endelevu na dhabiti zaidi, na inahitajika kwa dharura. “Pande zote zinapaswa kukutana na kujadiliana kutoa fursa kwa amani, ili watu hawa wote, mamilioni ya watu waliolazimika kuhama, waweze kurudi nyumbani au kuunganishwa na jamii mahali walipo, na waweze kuishi kwa amani pamoja kama jamii moja.”
  continue reading

100 Episoden

Artwork
iconTeilen
 
Manage episode 444122748 series 2027789
Inhalt bereitgestellt von UN Global Communications (Digital Solutions Unit) and United Nations. Alle Podcast-Inhalte, einschließlich Episoden, Grafiken und Podcast-Beschreibungen, werden direkt von UN Global Communications (Digital Solutions Unit) and United Nations oder seinem Podcast-Plattformpartner hochgeladen und bereitgestellt. Wenn Sie glauben, dass jemand Ihr urheberrechtlich geschütztes Werk ohne Ihre Erlaubnis nutzt, können Sie dem hier beschriebenen Verfahren folgen https://de.player.fm/legal.
Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC, imesalia katika mgogoro kwa miaka mingi, hali ambayo imewasababishia raia mateso ya hali ya juu zaidi yakiwemo mauaji, utekaji nyara, na kuteketezwa kwa nyumbaa zao. Mapigano hayo pia yamewafungisha viragozaidi ya watu milioni 6.4 nchini humo, na kulazimisha familia kutafuta usalama katika makazi ya muda yaliyojaa pomoni. Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi UNHCR limeonya kuwa mgogoro huu uliodumu kwa muda mrefu na ukiukwaji wa haki za binadamu ni mwiba kwa wakimbizi hawa wa ndani. Cicey Kariuki na taarifa zaidiRusayo ni eneo lililo na makazi ya muda ya wakimbizi mjini Goma katika Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Kongo. Miongoni mwa wakimibizi wa ndani wanaishi kwenye makazi haya ni Sebororo, mwanamke mwenye miaka 38 akitembea na watoto wake.Sebororo pamoja na wananawe watano wanaishi kwenye makazi ya pamoja na familia nyingine 90 huku wakisubiri kutengewa nyumba katika eneo hilo. Mama huyu anaeleza jinsi alivyojikuta katika makazi ya wakimbizi. Anasema,“tulianza kukimbia kuktoka kule tarehe tano mwezi wa kumi, awali walikuwa wanakuja lakini hawakuua watu, lakini leo hii wanaua watoto,wanaume na wanawake, sisi yalitushinda maanake wengine walikuwa pia wanatekweteza mimea.”Sebororo na watoto wake watano walitembea kwa wiki mbili kutafuta usalama, baada ya wapiganaji kuvamia kijiji chao cha Kiseguru katika Mkoa wa Kivu Kaskazini. Katika nusu ya kwanza ya mwaka wa 2024 pekee, zaidi ya watu 940,000 walilazimika kukimbia kutokana na ukatili, uliofanywa na makundi mengi yenye silaha yasiyo ya kiserikali huku familia nyingi zikifurushwa mara kadhaa. Kwa sasa anachokitamani zaidi Sebroro ni amani. “Haja yetu sisi ni watusaidie kwa kusimamisha vita ili turejee kwetu kwa sababu watu wanaisha.”Anasema.Kufurika kwa watu katika makazi haya ya muda kumezua wasiwasi mkubwa miongoni mwa wahudumu wa kibinadamu kufuatia hatari ya kuenea kwa magonjwa, ikiwa ni pamoja na virusi vya homa ya nyani au mpox.Ruven Menikdiwela, Kamishna Msaidizi wa Operesheni wa UNHCR ambaye alitembelea eneo hilo na kukutana na familia mbalimbali za wakimbizi na kusikiliza wasiwasi wao, anasema, “leo asubuhi, nilizungumza na mwanamke huyu ambaye ana watoto wadogo watano. Alitembea kwa wiki mbili kufika katika eneo hili, bado anasubiri huduma, bado anasubiri watoto wake watibiwe, na bado anasubiri chakula. Ninatambua kwamba hii ni hali ya kawaida kwa watu wote wanaoishi katika eneo hili. Kila mmoja ana majanga yake binafsi, kwa hivyo hizi siyo tu takwimu, bali kuna hadithi za kibinafsi nyuma ya kila moja ya hizi takwimu na majanga ya kibinafsi na majanga yanayoendelea pia, kwa sababu hatuoni suluhisho lolote kwenye mustakabali.”Katika ziara yake kwenye makazi haya, Ruven Menikdiwela, pia alifanya vikao na wadau kadhaa akiwemo Waziri mkuu, mamlaka za mkoa na mashirika ya umoja wa Mataifa. Ujumbe wake ulikuwa wazi kwamba amani ndiyo suluhisho endelevu na dhabiti zaidi, na inahitajika kwa dharura. “Pande zote zinapaswa kukutana na kujadiliana kutoa fursa kwa amani, ili watu hawa wote, mamilioni ya watu waliolazimika kuhama, waweze kurudi nyumbani au kuunganishwa na jamii mahali walipo, na waweze kuishi kwa amani pamoja kama jamii moja.”
  continue reading

100 Episoden

All episodes

×
 
Loading …

Willkommen auf Player FM!

Player FM scannt gerade das Web nach Podcasts mit hoher Qualität, die du genießen kannst. Es ist die beste Podcast-App und funktioniert auf Android, iPhone und im Web. Melde dich an, um Abos geräteübergreifend zu synchronisieren.

 

Kurzanleitung